Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 7 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 92 2023-04-14

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliauliza: -

Je, ni lini Kiwanda cha Mazava Winds Group – Morogoro kitapatiwa eneo kubwa la uwekezaji?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kiwanda cha Mazava Fabrics and Production East Africa Limited kinajishughulisha na uzalishaji wa nguo. Kiwanda hiki kipo chini ya mamlaka ya EPZ na kinafuata taratibu za uwekezaji zilizowekwa na Mamlaka hiyo. Kiwanda hiki kinatumia majengo ya kupanga kwa sasa.

Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya EPZ kwa kushirikiana na Mkoa wa Morogoro waliwezesha kupatikana kwa eneo la uwekezaji linalofahamika kwa jina la Star City lililopo Manispaa ya Morogoro, lenye ukubwa wa mita za mraba 20,000. Mwekezaji alikubaliana na eneo hili kuwa linafaa kwa ajili ya uwekezaji.

Mheshimiwa Spika, vilevile Mkoa wa Morogoro umetenga eneo la uwekezaji ambalo pia linafaa kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda liitwalo Kiyegera. Eneo hili linafaa kwa uwekezaji Mkubwa na Mdogo.