Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliauliza: - Je, ni lini Kiwanda cha Mazava Winds Group – Morogoro kitapatiwa eneo kubwa la uwekezaji?

Supplementary Question 1

MHE. NORA W. MZERU: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu mkubwa wa kutenga maeneo ambayo hayana migogoro na ardhi ili kuwaruhusu wawekezaji waweze kuwekeza kwenye maeneo hayo?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI:
Mheshimiwa Spika, ahsante, nilitaka kujibu swali ambalo ameliuliza Mheshimiwa Mbunge kuhusiana na masuala ya utengaji maeneo ya uwekezaji. Maelekezo ya Serikali katika mikoa yote na katika halmashauri zote ni kuhakikisha kwamba wanatenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji na maeneo yale lazima yatambuliwe ili yaweze kuwa tayari kwa ajili ya uwekezaji na kama kuna suala pengine la wananchi katika maeneo yale wanatakiwa waongee nao na waweze kuyamiliki kama ni halmashauri yenyewe au ni Serikali ya Kijiji ili muwekezaji anapopatikana kusiwe na mgogoro.

Mheshimiwa Spika, pia tunayo yale maeneo ya EPZ ambayo yapo yalikuwa yametengwa nayo yamewekwa kwa ajili ya uwekezaji. Kwa hiyo kwa maana ya Serikali tayari tunalitambua hilo katika kuepusha migogoro na wananchi. Na niombe Mbunge anione kama kuna eneo maalum ambalo pengine linahitaji maelezo ya ziada.