Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 7 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 93 2023-04-14

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: -

Je, ni kwa kiasi gani Mkoa wa Mtwara umewekeza na unanufaika na uchumi wa Bluu?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ili kuufanya Mkoa wa Mtwara kunufaika na uchumi wa bluu, Serikali imeimarisha miundombinu ya Bandari ya Mtwara na kuifanya kuwa ndiyo kituo kikuu cha usafirishaji wa bidhaa na malighafi mbalimbali. Serikali pia imejenga Kituo cha uzalishaji wa mbegu za mazao ya baharini (majongoo bahari, pweza, kamba na kadhalika) ili kuwasaidia wananchi wa mkoa huo.

Mheshimiwa Spika, vilevile Mamlaka ya Ufundi Stadi (VETA) inatoa mafunzo ya ufugaji wa majongoo bahari na kujenga vizimba vya ufugaji. Aidha, Serikali ya Mkoa wa Mtwara imeelekeza nguvu zake kwenye kilimo cha Mwani katika eneo la Naumo Wilayani Mtwara bila kusahau kilimo cha chumvi ya Bahari.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na jitihada za kuvutia wawekezaji katika uchumi wa Bluu nchini hasa katika sekta za usafirishaji baharini, kilimo, uvuvi, na utalii kwa ajili ya mikoa ya pwani ukiwemo Mkoa wa Mtwara.