Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 95 2023-04-17

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: -

Je, lini Serikali itawalipa fidia wananchi waliohamishwa kupisha maegesho ya malori eneo la Kurasini tangu mwaka 2015?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dorothy George Kilave, Mbunge wa Jimbo la Temeke, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa uthamini uliofanyika mwaka 2013 na ulipaji wa fidia kufanyika Mwaka 2015, Mwekezaji katika mradi huo alitoa shilingi bilioni 16.83 kwa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke kwa ajili kulipa fidia ambapo wananchi 165 waliofanyiwa uthamini ili kupisha mradi huo wamelipwa fedha zao kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya malipo hayo kukamilika, wananchi 44 kati ya 165 waliolipwa fidia hawakuridhika na malipo yaliyofanyika, hivyo wakafungua kesi ya madai ya mapunjo ya shilingi bilioni 3.198 katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kupitia Shauri Namba 50 la mwaka 2016. Tarehe 28 Mei, 2021, Mahakama ilitupilia mbali shauri hilo baada ya wananchi hao kushindwa kuthibitisha madai yao, hivyo, hakuna fidia inayodaiwa na maeneo yaliyotwaliwa kupisha ujenzi wa maegesho ya malori katika eneo la Kurasini kwani wananchi wote wamelipwa kwa mujibu wa sheria, ahsante.