Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, lini Serikali itawalipa fidia wananchi waliohamishwa kupisha maegesho ya malori eneo la Kurasini tangu mwaka 2015?

Supplementary Question 1

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali kwamba Mahakama imetupilia mbali suala hili, lakini je, hamuoni sasa iko haja ya Serikali na wananchi tukaweza kukaa pamoja tukapata uelewa wa pamoja ili wajue kwamba kweli walilipwa?

Swali la pili; je, yale maegesho ni lini sasa pataanza kujengwa maana bado pako wazi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dorothy Kilave Mbunge wa Jimbo la Temeke kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaona umuhimu wa kukaa na wananchi hawa katika kujenga uelewa wa pamoja ili kuondoa sintofahamu ya baadhi ya wanaodai kufikiri kwamba hawajalipwa. Kwa hiyo nikuhakikishie kwamba tutapanga utaratibu wa kwenda kuonana na wadai hao ili tuweze kuwapa uelewa wa pamoja wajue kwamba tayari walikwisha lipwa haki zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili, kujua lini ujenzi unaanza, naomba hili tulichukue kama Serikali tukalifanyie kazi tuweze kuona lini ujenzi huu unaanza, ahsante.