Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 97 2023-04-17

Name

Amina Daud Hassan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA DAUD HASSAN aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kufuatilia miradi ya TASAF iliyokamilika ili kuhakiki uendelevu wake?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Daud Hassan, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ili kuhakikisha kuwa miradi ya TASAF inakuwa endelevu, jamii huunda kamati ya matunzo na ukarabati ambayo jukumu lake ni kuweka sheria na taratibu za kusimamia matunzo na kuendeleza miradi hiyo. Mradi unapokamilika hubaki chini ya uangalizi wa wataalamu na TASAF wakishirikana na Halmashauri husika kwa kipindi cha miezi sita na baadaye mradi huo hukabidhiwa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri husika ambayo huendelea na jukumu la usimamizi, uendeshaji na matengenezo kwa kushirikiana na idara au taasisi inayohusika na miradi hiyo.