Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Daud Hassan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA DAUD HASSAN aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kufuatilia miradi ya TASAF iliyokamilika ili kuhakiki uendelevu wake?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA DAUD HASSAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali la nyongeza, ahsante Naibu Waziri kwa majibu ya Serikali mazuri na nina maswali yangu mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaongezea ruzuku wawezeshaji wakati wa malipo wakati wa masafa marefu ya kuwafikia walengwa?

Na swali la pili; shilingi 24,000 ni kidogo sana kwa wakati huu tulionao; je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaongezea ruzuku wanufaika wa mfuko wa TASAF?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Amina Daud Hassan kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali la kwanza juu ya kuongeza ruzuku; nataka nimhakikishie Mheshimiwa Amina, kwamba Serikali iko katika mchakato ikijadiliana na wadau mbalimbali wakiwemo wahisani wetu juu ya maslahi na utaratibu mzima wa miradi hii ya TASAF, hivyo hii ni moja ya agenda ambayo inakwenda katika mjadala. Juu ya jambo la udogo wa pesa inayotolewa; niseme Serikali imesikia jambo hili na katika mjadala unaoendelea kama nilivyoeleza katika swala la kwanza la nyongeza, ni kwamba Serikali nao wanajadiliana kuona jinsi gani tunaweza kuangalia kuongezea ruzuku kidogo kwa wafaidika ili kuweka mazingira mazuri ya wao kufaidika na mradi huo; ahsante sana.

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. AMINA DAUD HASSAN aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kufuatilia miradi ya TASAF iliyokamilika ili kuhakiki uendelevu wake?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa hii nafasi kuuliza swali la nyongeza. Katika halmashauri ya Wilaya ya Manyoni tulitenga kujenga Zahanati katika Kijiji cha Udimaa ambacho hakina Zahanati kupitia mradi wa TASAF.

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Zahanati ya Udimaa kwa kupitia mradi wa TASAF? Nashukuru.

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Chaya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi mingi inaibuliwa na wananchi, na sisi kama Wizara au Ofisi ya Rais inayosimamia miradi ya TASAF majukumu yetu ni kuchukua miradi hiyo na kuingiza kwenye mipango ya bajeti. Pale itakapopatikana bajeti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi wake huo tutakwenda kuufanyia kazi.