Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 98 2023-04-17

Name

Mohamed Abdulrahman Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukijenga upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Abdulrahman Mwinyi, Mbunge wa Chambani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, jengo la Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani ni chakavu na halifai kwa matumizi ya kutoa huduma za polisi. Mwezi Desemba, 2022 Serikali ilitoa kiasi cha fedha shilingi milioni 700 kwa ajili ya kujenga kituo cha polisi kipya cha Daraja B eneo hilo na taratibu za ujenzi zimeshaanza. Ujenzi unafanywa na Kikosi cha Ujenzi cha Polisi na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Agosti, 2023. Nashukuru.