Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Abdulrahman Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukijenga upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, kwanza niipongeza sana Serikali kwa hatua ambayo wamechukua na nina masuala mawili tu ya kuuliza.

(a) Kwa kuwa fecha zilitolewa Desemba, 2022 na mpaka leo imefika hatua ya kusafisha kiwanja hicho, je, ni tatizo gani ambalo linasababisha hilo?

(b) Ni lini Mheshimiwa Waziri atakwenda kuangalia ujenzi huo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mohabed Mwinyi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kuhusu tatizo la kuchelewa, ni kweli umetokea uchelewaji baada ya kubaini kwamba utaratibu uliokuwa umewekwa wa kutumia force account ulikosewa na baadhi ya watekelezaji wa jukumu hili. Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi alianza mfumo wa kuwaelimisha Makamanda wote wa Polisi wa Mikoa juu ya mfumo huo unaofanya kazi ili wauzingatie wakati wa utekelezaji, kwa hiyo ndio sababu ya kuchekelewesha. Sasa hivi wote umeshapitishwa ndiyo maana utekelezaji unaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti,kuhusu lini nitakwenda, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tunao utaratibu wa kufatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaofanywa na maofisa wetu lakini na sisi viongozi wa kisiasa tunapata nafasi tunaenda huko. Kwa hiyo itakapokuwa pengine Bunge hili linamalizika kabla ya mwezi Agosti Mbunge akiwa tayari niko tayari kuongozana nae kuangalie maendeleo ya ujenzi huo. Nashukuru sana.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukijenga upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo chetu cha Polisi cha Somanga kimechakaa sana.

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo kipya katika eneo hilo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ndulane kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kwamba ni kweli kituo cha Somanga ni cha muda mrefu na kimechakaa kama ilivyokuwa vituo vingi maeneo mbalimbali nchini. Tutakachofanya kabla ya kuki-condemn kituo hiki kwamba hakifai kwa matumizi ya binadamu tutaenda kufanya tathmini ya uchakavu wa kituo hiki. Iwapo itaonekana kuwa gharama za ukarabati ni kubwa au zinakaribia kulingana na gharama za ujenzi kitaingizwa kwenye mpango wa ujenzi wa kituo kipya, nashukuru.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukijenga upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani?

Supplementary Question 3

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa Kituo cha Makambako kimewakuta wananchi na wananchi walitoa eneo hilo kwa roho nyeupe;

Je, ni lini sasa Wananchi hao watalipwa ela zao kwa sababu mwaka jana Rais alipopita mwezi wa nane aliahidi na Mheshimiwa Naibu Waziri na Waziri alikuwepo, ni lini watalipwa wananchi hao ili wasiteseke fedha zao?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deo Sanga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kweli kwamba kituo cha Makambako kimekuta wananchi na uthamini ulishafanywa, na kuna takriban shilingi milioni 240 kwa ajiri ya kuwalipa fidia na kwa maagizo ambayo yameshatolewa na Mheshimiwa Rais wetu. Maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni ahadi ambayo lazima itekelezwe. Nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafatilia Wizara ya Fedha ili kupata fecha hizo za kulipa fidia ili wananchi hawa waweze kupata haki yao wapishe ujenzi wa kituo hiki, nakushukuru sana.