Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 99 2023-04-17

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: -

Je, Sheria za Tanzania zinasema nini kuhusu mahusiano ya jinsia moja?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru, na kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria sasa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Theonest kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria za Tanzania haziruhusu mahusiano ya jinsia moja. Kwa mujibu wa kifungu cha 9 cha Sheria ya Ndoa kinatafsiri ndoa ni mahusiano ya hiyari kati ya mwanaume na mwanamke. Aidha kwa mujibu wa kifungu cha 154 cha Sheria ya Kanuni za Adhabu, Sura ya 16 kinabainisha kuwa kufanya mapenzi kinyume na maumbile ya jinsia ni kosa la jinai ambalo adhabu yake ni kifungo cha maisha jela au kifungo kisichopungua miaka 30 jela.