Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, Sheria za Tanzania zinasema nini kuhusu mahusiano ya jinsia moja?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Sheria iko wazi kuzuia mahusiano na mapenzi ya jinsia moja, lakini tunaona kwenye vyombo vya habari watu wakitangaza na kujinasibu kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja.

Je, ni hatua kiasi gani zimefanyika kufikishwa Mahakamani ili tuweze kuzibiti kwa mujibu wa sheria? (Makofi)

Swali langu la pili, licha ya kuwepo kwa Sheria bado tumeona utekelezaji wake, pengine utekelezaji ndiyo umesababisha haya tunayoyasema.

Je, ni lini Serikali italeta mabadiliko ya sheria ili kila anayejihusisha, mwenye dalili na mwenye kufikiria aweze

kuchukuliwa hatua ili tuweze kulinda maadili ya nchi yetu? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anatropia Theonest kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge amependa kufahamu kwamba makosa hayo yanapojitokeza na watu wakijinasibu hadharani kwenye vyombo kama hatua zimekuwa zikichukuliwa? Hatua zimekuwa zikichukuliwa na ninyi ni mashahidi kwenye Bunge hili tumekuwa tukikemea jambo hili, nitoe rai kwa jamii kwamba jambo hili si la Serikali peke yake ni la jamii kwa umoja wetu ndiyo maana pale zinapokuwa zimebainika tumekuwa tukichukua hatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Mbunge anahitaji kujua kama tunaweza kufanya marekebisho ya sheria hizi? Sheria hizi zinafanya kazi kuhakikisha kwamba wale wanaobaninika wanachukuliwa hatua na ninyi ni mashahidi ndugu zangu hivi karibuni mahakama zetu zimetoa hukumu kwa watu ambao wamebainika wamefanya hivyo na wamekiri na wamefungwa miaka zaidi ya thelathini. Kwa hiyo, ni jukumu letu sote. Hata hivyo, pale ambapo utafiti utakuwa umefanyika Mheshimiwa Spika alielekeza kwamba utafiti wa kina ufanyike ili matendo haya yakibainika basi tuwe na kauli ya pamoja. Wakati huo ukifika kama marekebisho ya sheria yatahitajika Serikali ipo tayari.

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Niabu Waziri kwa majibu. Namwona Mheshimiwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Nape.

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kuongeza katika majibu yake mazuri.

Kwanza, hakuna matangazo ya mapenzi ya jinsia moja kwenye main media ambayo yanaruhusiwa na Serikali iko very strictly kwenye hili. Tulikuwa na chanagamoto kwenye online media ambayo mpaka sasa hivi jumla ya tovuti 334, akaunti za Facebook 361, Instagram 168, Twitter 12 na vikoa vya gay zaidi ya 2,456 vimefungiwa kwa sababu ya hatua hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, pamoja na hatua ambazo Serikali inachukua kufungia baadhi ya hizi online platforms lakini nadhani jambo hili bado liwe ni jukumu la jamii kuchukua hatua kuanzia kwenye familia na kuendelea sasa kwenye maeneo mengine. Nashukuru. (Makofi)