Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 100 2023-04-17

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaboresha bei ya ardhi inayotwaliwa na Migodi ili iendane na thamani ya ardhi ya eneo husika?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Mwikwabe Waitara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, bei ya soko la ardhi huandaliwa kwa kuzingatia Kifungu Na. 70 cha Sheria ya Uthamini na Usajili wa Wathamini ya mwaka 2016 pamoja na Kanuni Na. 53 ya Kanuni za Uthamini na Usajili wa Wathamini za mwaka 2018. Kanuni hiyo imeelekeza bei ya soko la ardhi kuzingatia visababishi vinavyoathiri bei ya soko la ardhi kati ya eneo moja na jingine na namna ya kufanya tafiti kwa kukusanya taarifa za soko la ardhi katika maeneo mbalimbali. Aidha, Kifungu cha (2) cha Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999 kimetafsiri kuwa petroli na aina zote za madini yanayopatikana chini ya ardhi siyo sehemu ya ardhi bali ni mali ya umma na hivyo umiliki wa ardhi hutolewa tofauti na leseni ya uchimbaji wa madini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na umuhimu wa kuhuisha viwango vya thamani ya ardhi na mali ili viendane na wakati, viwango vya bei ya soko la ardhi vimeboreshwa kwa kuzingatia sheria na kanuni za ardhi. Ahsante.