Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 101 2023-04-17

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: -

Je, nini matokeo ya utafiti wa mafuta uliofanyika katika Ziwa Tanganyika na lini mafuta yataanza kuchimbwa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng’enda, Mbunge wa Kigoma, Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, utafiti wa mafuta katika Ziwa Tanganyika umegawanyika katika vitalu viwili ambavyo ni Kitalu cha Kaskazini na Kusini. Kitalu cha Kaskazini kina ukubwa wa kilomita za mraba 9,430 ambapo mwaka 2015/2016, TPDC iliweza kukusanya, kuchakata na kutafsiri taarifa za uvutano wa sumaku ili kugundua maeneo yenye uwezekano wa kuwepo kwa mashapo ya kuhifadhi mafuta. Kitalu cha Kusini kina ukubwa wa kilomita za mraba 7,163 ambapo TPDC kwa kushirikiana na Mwekezaji - Kampuni ya Beach Petroleum waliweza kukusanya, kuchakata na kutafsiri taarifa za uvutano wa sumaku ili kubaini maeneo yenye uvutano na uwezekano wa kuhifadhi mafuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuwepo kwa viashiria vizuri vya uwepo wa mafuta katika vitalu vya Ziwa Tanganyika, matokeo ya mwisho kuhusu uwepo wa mafuta katika Ziwa hilo bado hayajapatikana kwa kuwa kazi ya utafiti bado inaendelea. Ahsante.