Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - Je, nini matokeo ya utafiti wa mafuta uliofanyika katika Ziwa Tanganyika na lini mafuta yataanza kuchimbwa?

Supplementary Question 1

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ninataka kujua kwa sababu viashiria vya uwepo wa mafuta kwenye Ziwa Tanganyika vimeonekana katika utafiti wa awali.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuharakisha utafiti huo ili kuweza kupata taarifa kamili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni lini wananchi wa Kigoma watarajie kupata taarifa za mwisho za utafiti huo ambao umechukua zaidi ya miaka mitano? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng’enda Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza katika swali la kwanza, mbinu ambazo zinafanywa na Serikali na jitihada zinazofanywa na Serikali kama mnavyofahamu Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameifungua sana Tanzania kwa ajili ya wawekezaji, nasi Wizara ya Nishati tumekuwa tukishiriki katika maonesho mengi ya Kimataifa kwa ajili ya kuwavutia wawekezaji kuja nyumbani kufanya kazi pamoja nasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua zinazofuata za utafiti ambazo zimebakia za 3D ni za gharama kubwa na Serikali imekuwa ikitafuta mbia wa kimkakati wa kushirikiana nae kwenye maeneo hayo ili kukamilisha utafiti huo ambao unatakiwa kufanyika. Mara tu baada ya kumpata na taarifa zikapatikana vizuri basi Ndugu zetu wa Kigoma na Watanzania kwa ujumla watapewa taarifa ya nini kimepataikana na lini uchimbaji wa mafuta katika Ziwa Tanganyika utaanza kufanyika. (Makofi)