Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 102 2023-04-17

Name

Geoffrey Idelphonce Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi mpya ya Mji wa Masasi ikiwa ni mradi funganishi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Mnivata?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Geoffrey Idelphonce Mwambe, Mbunge wa Masasi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa ushirikiano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika ipo katika hatua za mwisho za kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa kiwango cha lami kwa barabara ya Mnivata – Newala – Masasi yenye urefu wa kilomita 160. Taarifa ya uchambuzi wa zabuni za kumpata mkandarasi zimekamilika na kuwasilishwa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa ajili ya kupata idhini ya kuendelea na hatua ya kusaini mkataba (no objection). Kwa vile mradi wa ujenzi wa Stendi mpya ya Mji wa Masasi ni moja ya miradi itakayotekelezwa kama mchango kwa jamii chini ya mradi wa ujenzi wa barabara hii, kazi za ujenzi wa stendi mpya ya Mji wa Masasi itaanza baada ya mkataba wa ujenzi wa barabara kusainiwa na kazi za ujenzi kuanza. Ahsante.