Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Geoffrey Idelphonce Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi mpya ya Mji wa Masasi ikiwa ni mradi funganishi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Mnivata?

Supplementary Question 1

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE. Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, ninataka nijue ni lini basi Serikali ina uhakika wa kupata hii (No objection) kutoka kwa Benki ya Maendeleo ya Afrika ili tujue kwa uhakika kabisa ni lini tutaanza utekelezaji wa mradi huu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ninataka kufahamu ni lini Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya Wilaya ya Temeke itajenga stendi mpya kwa ajili ya mabasi ya kutoka Mtwara, Lindi na Ruvuma yanayoingia Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya Dual Carriage Way ya kutoka Dar es Salaam kwenda Mkuranga?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Geoffrey Mwambe, Mbunge wa Masasi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu za manunuzi zinakwenda vizuri na ni matumaini yetu kwamba kama wenzetu watakwenda kama tulivyopanga tunategemea tutapata (No objection) kwa sababu taratibu zote karibu zimekamilika. Sasa ni lini? Kwa kweli tutanategemea wenzetu wa African Development Bank watakavyokuwa wamefanya kazi yao kwa uharaka na kutoa hiyo (No objection) na sisi tutaanza kutangaza hiyo kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kujenga stendi, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi kama wizara kwa kushirikiana na wenzetu wa TAMISEMI ambao hasa ndio wanaoshughulikia stendi hizi za mijini, tutakaa pamoja tuone uwezekano wa kujenga hiyo stendi na hasa tu nikimhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa upande huo tayari tuna utaratibu wa kuja na mpango wa kujenga dual carriage way ya kutoka Mbagala – Kongowe na ikiwezeka mpaka Vikindu. Ahsante.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi mpya ya Mji wa Masasi ikiwa ni mradi funganishi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Mnivata?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE D. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, je, ni lini barabara ya kutoka Waso kwenda Loliondo yenye urefu wa kilometa 10 itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Arusha, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ile ilikuwa ni ahadi na agizo la Mheshimiwa Rais, hivi tunavyoongea tayari tenda ilikwishatangazwa ya kujenga kilometa hizo 10 za kutoka Waso hadi Loliondo kwa kiwango cha lami.

Name

Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi mpya ya Mji wa Masasi ikiwa ni mradi funganishi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Mnivata?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi hii, kwa kuwa ipo ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa stendi ya kisasa katika Mji wa Mwanga, swali langu ni je, ni lini ahadi hii ya Mheshimiwa Rais itatekelezwa kwa wananchi wa Mwanga? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tadayo, Mbunge wa Mwanga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Tadayo aniruhusu niweze kupata maelezo sahihi ya kuhusu utekelezaji wa hii ahadi ya Mheshimiwa Rais kwa TANROADS kujenga hii stendi ya kisasa katika Mji wa Mwanga baada tu ya kutoka kwenye kipindi hiki. Ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi mpya ya Mji wa Masasi ikiwa ni mradi funganishi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Mnivata?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa barabara ya kutoka Bariadi – Itilima – Meatu – Sibiti mpaka Singida iko kwenye ilani. Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii barabara ni sehemu ya Barabara ambayo ni ya kutoka Maswa – Sibiti Kwenda Haidong ambayo ipo kwenye mpango wa EPC+F na nimekwisha itolea maelezo mengi kwamba tayari taratibu zinaendelea na sasa tayari upande wa Wizara ya Ujenzi tumemaliza sasa tumekwishapeleka kwa wenzetu Wizara ya Fedha kuweza kupitia mapendekezo yetu. Ahsante.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi mpya ya Mji wa Masasi ikiwa ni mradi funganishi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Mnivata?

Supplementary Question 5

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kutoka Mwenge kuelekea Bagamoyo imekuwa na msongamano mkubwa na kusababisha Shughuli za kiuchumi Mkoa wa Dar es Salaam kusimama. Ni lini sasa Serikali itajenga barabara ya Mabwepande kuelekea Mbezi Jimbo la kibamba ili kuweza kupunguza foleni hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara ya kutoka Mwenge kwenda Mabwepande ni BRT number Four ambayo iko katika hatua za manunuzi, lakini barabara aliyoitaja itakuwa ni moja ya barabara za kupunguza msongamano lakini pia kwenda kwenye hii stendi mpya na iko kwenye mpango wa kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.