Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 104 2023-04-17

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA K.n.y. MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: -

Je, nini kimesababisha mbolea kuadimika na kuleta hasara kwa Wakulima na Wawekezaji nchini katika msimu wa mwaka 2022/2023?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Luhaga Joelson Mpina, Mbunge wa Kisesa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nchi katika msimu wa kilimo wa mwaka 2022/2023 hatukuwa na uhaba wowote wa mbolea. Vilevile Serikali haijapokea malalamiko yoyote kutoka kwa wakulima na wawekezaji yanayohusu kupata hasara kutokana na kuadimika kwa mbolea. Changamoto pekee ilijitokeza ilikuwa ni mwamko mkubwa wa wakulima kuhitaji kununua mbolea kuliko uwezo wa mtandao wa mawakala, ambapo Serikali imeendelea kuipatia ufumbuzi na kuongeza idadi ya mawakala kutoka 1,392 mwezi Agosti, 2022 hadi 3,265 mwezi Machi, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, makadirio ya mahitaji ya mbolea kwa msimu wa 2022/2023 yalikuwa ni tani tani 667,730 na hali ya upatikanaji wa mbolea hadi kufikia mwezi Machi, 2023 umefikia tani 748,890 sawa na asilimia 112 ya mahitaji ya mbolea ndani ya nchi, ikilinganishwa na kipindi kama hicho kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2021/2022.