Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA K.n.y. MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: - Je, nini kimesababisha mbolea kuadimika na kuleta hasara kwa Wakulima na Wawekezaji nchini katika msimu wa mwaka 2022/2023?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Mpina.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango gani wa kutoa ruzuku ya mbolea kwa wakulima wa tumbaku? Hilo swali la kwanza. Swali la pili: Je, Serikali inajipangaje kuhakikisha wakulima wanapata mbolea mapema ili kuweza kuwaruhusu mazao yote yale ya umwagiliaji yaweze kupata mbole kwa wakati?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika mpango wa msimu uliomalizika, wakulima wa zao la tumbaku hawakuwepo katika mpango wa ruzuku kwa sababu katika utaratibu wa manunuzi ya pembejeo kwenye sekta hii ya tasnia ya tumbaku wamekuwa na utaratibu maalum ambao ulianza kabla ya mfumo wa ruzuku. Hata hivyo, tumeendelea kukaa nao kuangalia pia utaratibu bora ili na wao waweze kunufaika na utaratibu wa ruzuku ambao unaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili la kuhusu mbolea kupatikana mapema; tumeshakaa na waagizaji na wazalishaji wa mbolea wote hapa nchini kuhakikisha kwamba kuanzia mwezi wa Saba mbolea ianze kuingizwa nchini ambayo itawakuta wakulima wakiwa bado na uwezo wa kununua kwa kuwa watakuwa wamevuna ili wakulima wetu itakapofika kipindi cha kuanza msimu mbolea iwepo yote hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumebaini upungufu katika msimu uliopita, tumeyarekebisha, tutahakikisha kwamba wakulima wanapata mbolea kwa wakati katika msimu ujao.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA K.n.y. MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: - Je, nini kimesababisha mbolea kuadimika na kuleta hasara kwa Wakulima na Wawekezaji nchini katika msimu wa mwaka 2022/2023?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA HASSAN TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa nchi yetu ina mifugo mingi ya kutosha, hivyo uwezekeno wa kuwa na mbolea ya samadi ni mkubwa, nini mkakati wa Serikali katika kuboresha na kuhamasisha matumizi ya mbolea ya samadi ili ilete tija? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa kwa hapa Dodoma tunacho kiwanda cha mbolea kinaitwa ITRACOM ambacho kinazalisha mbolea inayoitwa Organo Mineral ambapo zaidi ya asilimia 50 wanatumia samadi na imekuwa kichocheo kikubwa na soko la uhakika kwa wafugaji wetu wengi hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba ilikuwa ni mkakati wa Serikali, na kiwanda kipo hivi sasa na kinatumia malighafi hiyo kama sehemu ya kutengeneza mbolea hapa nchini.

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA K.n.y. MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: - Je, nini kimesababisha mbolea kuadimika na kuleta hasara kwa Wakulima na Wawekezaji nchini katika msimu wa mwaka 2022/2023?

Supplementary Question 3

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Uchache wa mawakala ulileta usumbufu wa upatikanaji wa mbolea kwa msimu uliopita. Je, Serikali haioni haja ya kupeleka mawakala angalau kwa kila kijiji ili wasiendelee na usumbufu walioupata wakulima kwa msimu uliopita? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya changamoto ambazo pia tulizibaini wakati wa msimu uliopita ilikuwa ni hiyo ya uchache wa mawakala. Tumeshatoa maelekezo kupitia TFRA kuongeza idadi ya usajili wa Mawakala ili wakulima wapate mbolea katika maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, tumeamua kuyatumia maghala yote makubwa ya Serikali kwa ajili ya uhifadhi na kupeleka mbolea karibu na wakulima; na tatu, tumeruhusu Vyama vya Ushirika pia kuwa sehemu ya Mawakala ili kufanya huduma hii ifike kwa ukaribu zaidi kwa wakulima.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA K.n.y. MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: - Je, nini kimesababisha mbolea kuadimika na kuleta hasara kwa Wakulima na Wawekezaji nchini katika msimu wa mwaka 2022/2023?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Uhalisia wa upatikanaji wa mbolea kwa wakti kwa wakulima wetu bado ni changamoto kubwa; na inasemekena mbolea hizi zinatumika kusafishia madini kwenye migodi. Sasa nilitaka kujua, ni Serikali itafanya tafiti za kina kujua matumizi ya ziada ya mbolea hizi nje ya kilimo ili kuweza kuwa na bajeti halisia ya kuwafikia wakulima kwa wakati kulimo ilivyo hivi sasa? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, matumizi ya msingi ya mbolea yanafahamika, ni kwa ajili ya kilimo. Kama kuna jambo lingine la ziada kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema, sisi na wenzetu wa madini tutakaa tushirikiane ili kuweza kulifanyia utafiti wa kina na kuweza kupata majibu stahiki katika eneo hili ili mwisho wa siku tuwe na mbolea kwa mahitaji halisi yanayohitajika katika kilimo chetu cha msingi Tanzania. (Makofi)