Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 105 2023-04-17

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha mapitio ya kubaini madawa na vihatirishi vinavyosababisha madhara na vinaendelea kutumika katika Kilimo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania hutekeleza utaratibu wa kubaini viuatilifu na vihatarishi vinavyosababisha madhara kwa mazao, mimea na afya ya binadamu na wanyama. Utaratibu huo hufanyika kulingana na kifungu cha 54 cha Sheria Na. 4 ya Afya ya Mimea ya mwaka 2020 kinachompa Mamlaka Msajili wa viuatilifu nchini kufuta usajili wa viuatilifu vinavyosababisha madhara kwa afya ya binadamu na mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2018 hadi 2021, Serikali ilifanya mapitio ya kubaini viuatilifu vyenye madhara makubwa kwa afya ya binadamu na mazingira vijulikanavyo kama Highly Hazardous Pesticides. Mapitio hayo yalibaini aina ya viuatilifu 44 vyenye viambata amalifu vyenye madhara kwa afya ya binadamu na mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia hatua hiyo, Serikali kupitia TPHPA imeanza kuchukua hatua za kusitisha matumizi ya viuatilifu 44 vilivyobainika na inaendelea kufanya kaguzi za mara kwa mara katika maghala na maduka ya viuatilifu ili kubaini uwepo wa viuatilifu vingine vyenye madhara.