Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha mapitio ya kubaini madawa na vihatirishi vinavyosababisha madhara na vinaendelea kutumika katika Kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Nashukuru sana kwa majibu ya Serikali; pamoja na kitu kizito alichopigwa nacho Mheshimiwa Naibu Waziri jana Mkapa, lakini anaweza kutoa majibu ya kina. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali imefanya uhakiki kwamba viuatilifu hivi 44 vilivyobainishwa vimeweza kutokomezwa na kwamba notice ya katazo au ya ku- deregister au zuio inabainika kwa uwazi na kwa ufasaha kabisa kwa wanunuzi, watumiaji na wanaohusika wote? (Makofi)

Mheshimwa Mwenyekiti, swali lingine: Je kuna mpango gani wa Serikali kupima mboga mboga zinazoingia sokoni na kuwajulisha watumijai na walaji kama vile tunavyofanya kwa mazao yanayouzwa nchi za nje? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza kwa mujibu wa Sheria Na. 4 ya Afya ya Mimea ya Mwaka 2020, ni wajibu wa kimsingi wa mamlaka kuhakikisha kwamba inafanya kaguzi za mara kwa mara ili kuweza kubaini viuatilifu ambavyo vimesitishwa na kuweza kuchukua hatua sambamba na kutoa taarifa kwa watumiaji ili isiweze kuleta madhara zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili la kuhusu upimaji wa mazao ya mboga mboga, Serikali inapima uwepo wa masalia ya viuatilifu vilivyotokomezwa katika mazao yote. Hivi sasa tumenunua Rapid Test Kit ambayo pia itasaidia kupima masalia ya viuatilifu katika mazao ya mboga mboga ili kuweza kumlinda mtumiaji. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo pia tunahamasisha na kilimo hai, kuondokana na changamoto hizi ambazo zinajitokeza na matumizi ya viuatilifu.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha mapitio ya kubaini madawa na vihatirishi vinavyosababisha madhara na vinaendelea kutumika katika Kilimo?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kumekuwa kuna changamoto kwa wakulima hasa wa zao la mahindi msimu huu, mahindi yamevamiwa na wadudu lakini mkulima anatumia dawa nne, sita mpaka nane, anazichanganya lakini bado hazi-react kwa wadudu hao na elimu kwa wananchi wetu bado ni ndogo: Nini mkakakti wa Serikali kuhakikisha kwamba dawa sahihi kulingana na wadudu husika ambao wamevamia mazao inapata tiba kwa wananchi wetu? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Mamlaka ya Afya ya Mimea na viuatilifu (TPHPA) Serikali imekuwa na utaratibu wa kuhakikisha kwamba viuatilifu vyote vinavyoingizwa nchini ni vile ambavyo vinakidhi mahitaji na matakwa ya changamoto ambazo zinawakabili wakulima wetu. Hivyo ambacho tutakifanya zaidi, ni kuendelea pia kutoa elimu kwa wakulima wetu juu ya matumizi sahihi ya viuatilifu hivi ili viweze kuleta matokeo chanya na viweze kumsaidia mkulima katika kupambana na uhalibifu wa mazao.

Mheshimiwa, Mwenyekiti, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba Serikali inatambua changamoto zilizojitokeza na kuendelea na ukaguzi ili tukibaini kwamba kuna changamoto kama hiyo katika baadhi ya maeneo, tutaweza kuchukua hatua stahiki na tuweze kufuta mpaka usajili katika wale ambao wanahusika. Sambamba na hili, uhakika tu ni kwamba tutahakikisha kwamba mkulima wetu anapata viuatilifu ambavyo ni sahihi kwa wadudu sahihi.