Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 106 2023-04-17

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA K.n.y. MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuondoa tofauti ya Viwango vya Ufaulu kwa Mitihani ya Kidato cha Nne na Sita Kati ya Bara na Zanzibar?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Said Issa, Mbunge wa Konde kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchambuzi wa jumla wa matokeo ya mitihani ya Kidato cha Nne na Sita uliofanywa na Baraza la Mitihani la Tanzania katika kipindi cha mwaka 2013 hadi 2022 ulibainisha kuwa Zanzibar ilikuwa na ufaulu wa juu zaidi kwa kidato cha nne na sita kuliko Tanzania Bara katika mwaka 2013, 2015 na 2016. Aidha, Tanzania Bara ilikuwa na ufaulu wa juu zaidi ya Zanzibar kwa mwaka 2014 na mwaka 2017 hadi 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, usimamizi na uendeshaji wa elimu ya msingi (awali, msingi na sekondari) siyo suala la Muungano, ingawa kwa Kidato cha Nne na cha Sita wote wanafanya mtihani mmoja wa Baraza la Mitihani la Tanzania. Kwa msingi huo, kila upande wa Muungano una mikakati yake ya namna ya kuongeza kiwango cha ufaulu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali inaendelea na mapitio ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 na Mitaala ya Elimu. Zoezi hili linafanyika kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa lengo la kuhakikisha kuwa tunakuwa na Sera na Mitaala inayolenga kutoa ujuzi zaidi kwa wahitimu na pia tunaoanisha kwa kiwango kikubwa elimu inayotolewa Tanzania Bara na ile inakayotolewa Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.