Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA K.n.y. MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuondoa tofauti ya Viwango vya Ufaulu kwa Mitihani ya Kidato cha Nne na Sita Kati ya Bara na Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na mikakati ya Serikali ambayo imeianisha lakini bado kuna changamoto ya ufaulu hasa katika masomo ya sayansi na hisabati. Ni nini mkakati wa Serikali kupandisha ufaulu huo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, najua kuna mchakato unaendelea wa kuiangalia mitaala. Je, ni lini hiyo mitaala mipya itatumika katika sehemu zote mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Khalifa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza, anataka kufahamu juu ya mkakati wa Serikali hasa hasa katika masomo ya hisabati na sayansi. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, Serikali tumejipanga vizuri kwa kufanya mambo yafuatayo: -

(i) Kuweka kipaumbele hasa hasa kwenye ajira za walimu wa masomo haya ya sayansi pamoja na hisabati;

(ii) Kuhakikisha kwamba tunakwenda kujenga maabara katika shule zetu ambazo zinazotoa masomo haya ya sayansi;

(iii) Kuhakikisha kwamba tunapeleka vifaa vya kujifunzia na kufundishia kwa ajili ya ufundishaji wa masomo haya; na

(iv) Kuendelea kuhakikisha walimu wale wa masomo ya sayansi basi tunawapeleka kwenye mafunzo ili kuhakikisha kuwajengea uwezo wa kuweza kufundisha masomo haya kwa umahiri, kwa umahiri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili anataka kufahamu utaratibu wa mitaala. Ni kweli tumezungumza hapa kwamba tunaendelea na uratibu pamoja na maboresho ya mtaala wa mwaka 2014.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge pamoja na Bunge lako Tukufu, mitaala yetu pamoja na sera tayari tuna rasimu ya nyaraka hizo na hivi sasa taratibu zinazoendelea ni kuendelea kupata maoni ya wadau ikiwemo na ninyi Waheshimiwa Wabunge. Tutaleta rasimu hiyo katika Bunge lako Tukufu ili kuweza kupata ridhaa na baadaye kwenda kwenda kwenye mamlaka zinazohusika na ithibati au kupitisha mitaala hii pamoja na sera ili iweze kuanza kutumika. Kwa hiyo, mara baada ya mchakato huu kukamilika, mitaala hii itaanza kutumika rasmi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.