Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 108 2023-04-18

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza:-

Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa madaraja ya Mto Piyaya Kata ya Piyaya na Mto Juhe Kata ya Samunge?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Shangai, Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Madaraja ya Mto Piyaya na Mto Juhe ambayo yana urefu wa zaidi ya mita 80. Aidha, ujenzi wa madaraja hayo unahitaji kuanza na kazi ya usanifu wa kina ikiwemo uchambuzi wa miamba, ili kupata gharama halisi ya ujenzi wake.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2024/2025, Serikali itafanya usanifu wa kina wa madaraja haya, ili kupata gharama halisi ya ujenzi. Vilevile, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya barabara za Jimbo la Ngorongoro ikiwemo ujenzi wa madaraja kadri ya upatikanaji wa fedha.