Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza:- Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa madaraja ya Mto Piyaya Kata ya Piyaya na Mto Juhe Kata ya Samunge?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Spika, nashukuru, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza. Je, Serikali imetenga kiasi gani cha fedha kwa ajili ya usanifu kwa madaraja yote mawili ya Mto Juhe na Piyaya kwa mwaka wa fedha 2023/2024?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; nini commitment ya Serikali pindi upembuzi utakapokamilika kutenga fedha haraka kwa sababu, madaraja haya yatakayojengwa yatasaidia kuokoa maisha ya watoto ambao wamekuwa wakichukuliwa na maji ya Mto Juhe pamoja na Mto Piyaya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA – (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Emmanuel Shangai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimetoa majibu hapa kwenye majibu yangu ya msingi. Serikali itatenga fedha katika mwaka wa 2024/2025 ili kuhakikisha usanifu unafanyika katika madaraja haya ya Mto Piyaya na Mto Juhe.

Mheshimiwa Spika, lakini katika swali lake la pili; Serikali imeweka kipaumbele sana katika kuhakikisha inatengeneza barabara na madaraja katika Jimbo la Ngorongoro, lakini katika majimbo yote ya hapa nchini. Na tayari maelekezo yalikuwa yameshakwenda kwa mameneja wote wa TARURA wa Wilaya kuhakikisha wanatenga bajeti katika barabara hizi ambazo ni za kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, na ni imani yangu katika bajeti hii, barabara hii itakuwa nayo imetengewa fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu. Naomba kuwasilisha.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza:- Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa madaraja ya Mto Piyaya Kata ya Piyaya na Mto Juhe Kata ya Samunge?

Supplementary Question 2

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, nil in Daraja la Isararo – Ipanzya litajengwa, ambayo imekuwa ni ahadi ya muda mrefu sana?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika,
naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hassunga, la ahadi ya kujenga madaraja haya ambayo ameyataja: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimekuwa nikimjibu Mheshimiwa Shangai hapa; maelekezo yalitoka kwa mameneja wote wa TARURA wa mikoa na wote wa Wilaya kuhakikisha barabara hizi ambazo pia ni ahadi za viongozi lakini, lakini ambazo ni kipaumbele katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu yatengewe fedha. nitakaa na Mheshimiwa Mbunge kuweza kuangalia katika ahadi hizi na barabara hii kama imetengewa fedha.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza:- Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa madaraja ya Mto Piyaya Kata ya Piyaya na Mto Juhe Kata ya Samunge?

Supplementary Question 3

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza: -

Je, Serikali iko tayari kutenga fedha kwa ajili ya kutengeneza Daraja la Sanjawe, Mara na Daraja linalounganisha Basodeshi na Gietamo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika,
naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Samweli, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo tayari kutenga fedha ya barabara hii ya Sandawe. Na ninaamini katika mwaka huu wa fedha tayari TARURA, kupitia Meneja wa Mkoa na Meneja wa Wilaya, watakuwa wameiwekea fedha barabara hii na tutampatia Mheshimiwa Mbunge Taarifa hiyo.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza:- Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa madaraja ya Mto Piyaya Kata ya Piyaya na Mto Juhe Kata ya Samunge?

Supplementary Question 4

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza: -

Je, ni lini Serikali itajenga daraja linalounganisha Kata ya Kiwele, Kijiji cha Kiwele na Kata ya Nzihi, Kijiji cha Kipera?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Kiswaga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokuwa nimeshasema hapo awali, tayari maelekezo yalikuwa yametolewa kwa mameneja wote wa TARURA wa mikoa na Wilaya kuhakikisha wanatenga fedha kwenye barabara hizi na madaraja haya ambayo ni viunganishi vya kata na kata na Wilaya na Wilaya. Na ninaamini katika barabara ambayo Mheshimiwa Kiswaga ameitaja nayo Meneja wa TARURA Mkoa na Wilaya watakuwa nayo wameifanyia kazi.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza:- Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa madaraja ya Mto Piyaya Kata ya Piyaya na Mto Juhe Kata ya Samunge?

Supplementary Question 5

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, ni zaidi ya miaka mitano sasa daraja la kuunganisha Kata ya Msolwa Station na Mang’ula limekatika sambamba na kivuko cha Chikago – Kidatu na kivuko cha pale Kiberege. Je, ni lini Serikali itajenga madaraja haya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA – (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asenga: -

Mheshimiwa Spika, naomba nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumuelekeza Meneja wa TARURA wa Mkoa wa Morogoro na Meneja wa TARURA wa Wilaya anakotoka Mheshimiwa Asenga, kuhakikisha wanafika kwenye barabara hiyo ambayo ameitaja Mheshimiwa Asenga, ili kufanya tathmini na kujua ni kiasi gani kinahitajika kwa ajili ya kuweza kuunganisha kata hizo mbili.