Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 109 2023-04-18

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka fedha za ukarabati wa Madarasa, Mabweni na Usafiri katika Shule ya Sekondari ya Geita?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha wa 2020/2021, Halmashauri ya Mji Geita ilitumia fedha za ndani shilingi milioni 50 kukarabati mabweni matatu ya Shule ya Sekondari ya Geita. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, shilingi milioni 20 kutoka fedha za CSR zilitumika kukarabati mabweni mawili, shilingi milioni 100 zilitumika kujenga bweni moja na shilingi milioni 40 zilitumika kujenga madarasa mawili mapya. Vilevile katika mwaka 2022/2023, Serikali imepeleka shilingi milioni 360 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mapya matatu katika shule hiyo.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kupeleka fedha za ukarabati kwa shule za kitaifa ikiwemo Shule ya Sekondari ya Geita pamoja na ununuzi wa magari kwa ajili ya shule za mabweni kulingana na upatikanaji wa fedha.