Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha za ukarabati wa Madarasa, Mabweni na Usafiri katika Shule ya Sekondari ya Geita?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri: -

Mheshimiwa Spika, umri wa shule hii nilisoma kwenye shule hiyo, kwa hiyo, imechakaa sana. Ni lini Serikali itatuma timu maalum kwenda kutathmini miundombinu ya shule hii?

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili; shule hii ambayo ina O- Level na A-Level haina kabisa mwalimu wa physics, haina kabisa mwalimu wa biology na ina walimu wa mkataba wa geography na history. Naomba commitment ya Waziri kwenye mgawo wa walimu wanaoajiriwa hivi karibuni, shule hii itapata walimu wa kutosha?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa amekuwa akifuatilia sana suala la shule hii ya sekondari ya Geita ambayo ni ya kitaifa. Nikienda kwenye swali lake la kwanza la, ni lini timu itafika katika shule hii kufanya tathmini.

Mheshimiwa Spika, nimuahidi kwamba, baada ya Bunge hili Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, itahakikisha timu inafika katika shule hii na kufanya tathmini na kuweza kuleta taarifa yake, ili kuweza kuifanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, lakini nikienda kwenye swali lake la pili, la lini Serikali itapeleka walimu: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo wote ni mashahidi humu ndani, Serikali imetangaza ajira zaidi ya 21,000 kwa walimu na watumishi wa sekta ya afya. Na tutahakikisha shule hii vilevile inapata walimu hawa wa sayansi ambao amewataja Mheshimiwa Mbunge.