Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 111 2023-04-18

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: -

Je, ni Wazee wangapi wamepewa Bima ya Wazee na waliobaki ni lini watapewa Bima hizo Wilayani Kakonko?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Jimbo la Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko inatekeleza afua mbalimbali za afya ikiwemo huduma za afya kwa wazee, kwa kuwapatia vitambulisho vya matibabu bila malipo wazee wenye umri wa miaka 60 na kuendelea wasio na uwezo, kama ilivyo katika Sera ya Wazee ya mwaka 2003, Sera ya Afya ya mwaka 2007 na Mwongozo wa uchangiaji wa huduma za afya nchini.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko iliwatambua wazee wa miaka 60 na kuendelea wasio na uwezo wapatao 11,524. Kati yao wazee 6,084 walipewa vitambulisho vya matibabu bila malipo, wazee 2,000 walikatiwa bima ya mfuko wa afya ya jamii ulioboreshwa kupitia mapato ya ndani.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha wa 2023/2024, Serikali kupitia mapato ya ndani itatenga bajeti kwa ajili ya kuwapatia vitambulisho wazee 3,440 waliobaki katika Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko.

Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kuwakumbusha viongozi wote wa mikoa na halmashauri kutekeleza maelekezo ya kuwapa vitambulisho vya matibabu bila malipo wazee wote wenye umri wa miaka 60 na kuendelea wasio na uwezo. ahsante.