Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, ni Wazee wangapi wamepewa Bima ya Wazee na waliobaki ni lini watapewa Bima hizo Wilayani Kakonko?

Supplementary Question 1

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, tatizo lililopo ni kwamba, hata wale ambao wameshapata vitambulisho hawapewi huduma inayostahili kadiri ya utaratibu uliopo. Nini kauli ya Serikali kwa hawa ambao wamepata vitambulisho, lakini hawapati huduma ambayo wanastahili?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; lini sasa hawa waliobaki 3,440 nao watapata vitambulisho?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika,
naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Jimbo la Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshaelekeza kuhakikisha kila halmashauri kwanza inaandikisha na kuwapa vitambulisho wazee
wote wenye umri wa miaka 60 na kuendelea, wasio na uwezo, lakini inatenga dirisha kwa ajili ya huduma kwa wazee na kuhakikisha kwamba, dawa zote muhimu zinapatikana kwa ajili ya wazee. Kwa hiyo, naomba nitoe Kauli ya Serikali kwamba, wakurugenzi wote wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wahakikishe maelekezo ya Serikali yanatekelezwa na wazee wetu wapate huduma kama inavyostahiki.

Mheshimiwa Spika, lakini pili, kuhusu vitambulisho kwa wazee waliobaki, kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi kwamba, mwaka ujao wa fedha Halmashauri watatenga fedha kwa ajili ya kuwapa vitambulisho wazee waliobaki 3440.