Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 115 2023-04-18

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: -

Je, lini mpaka wa Hifadhi ya Ugalla utarekebishwa ili kurejesha kwa wananchi eneo walilokuwa wanatumia kwa ufugaji?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Jimbo la Urambo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Hifadhi ya Taifa Ugalla ilianzishwa kwa Sheria ya Hifadhi za Taifa, Sura 282 baada ya kupandisha hadhi Pori la Akiba Ugalla kwa Tangazo la Serikali, G.N. No. 936 la mwaka 2019.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa eneo hili ni muhimu kiuhifadhi na ndani yake kuna vyanzo vya maji, kabla ya kubadilishwa hadhi eneo hili lilihusisha shughuli za uvunaji zikiwemo ufugaji nyuki na uvuvi. Hali hii ilileta changamoto za kiuhifadhi ikiwemo uchomaji moto unaoathiri uoto wa asili na uchafuzi wa vyanzo vya maji. Hivyo, Serikali haioni haja ya kufanya marekebisho ya mpaka wa Hifadhi ya Taifa Mto Ugalla.