Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - Je, lini mpaka wa Hifadhi ya Ugalla utarekebishwa ili kurejesha kwa wananchi eneo walilokuwa wanatumia kwa ufugaji?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Swali la kwanza; je, Serikali yetu sikivu ninavyoielewa mimi, haioni umuhimu wa kujenga mahusiano mema kati ya hifadhi na wananchi kwa kuwapa eneo la kuweka mizinga yao na kufuga mifugo yao kama walivyozoea na hasa kutokana na ongezeko la watu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; hivi Serikali haioni kuna haja ya kumaliza suala ambalo linaulizwa kila mwaka kwa kulipatia ufumbuzi wa kudumu?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika,
ahsante. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Jimbo la Urambo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niahidi tu kwamba tutaangalia maeneo mengine yaliyo jirani na eneo hilo ili warinaji wa asali, hususan wale wafugaji wa nyuki, tuweze kuwahamisha ili tuwapeleke katika misitu ambayo inaendana na uhifadhi wa mazingira yanayohusiana na ufugaji nyuki.

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - Je, lini mpaka wa Hifadhi ya Ugalla utarekebishwa ili kurejesha kwa wananchi eneo walilokuwa wanatumia kwa ufugaji?

Supplementary Question 2

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Timu ya Mawaziri Nane ilikuja katika Kata ya Kigwa na kutuahidi kutupa eneo katika Kigwa Rubuga. Je, ni lini Serikali itaweka mipaka mipya katika maeneo hayo ili wananchi wajue mipaka yao?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika,
ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tulikuwa na kazi ya kufanya tathmini, kamati hii iliandaliwa na Kamati ya Mawaziri Nane na tayari wengi wameshamaliza kazi yake. Kazi inayofanyika sasa hivi ni kuainisha mipaka na kuweka vigingi. Hivyo, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Igalula kwamba wakati wowote tutaendelea kufanya kazi ya kuweka vigingi.