Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 9 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 119 2023-04-18

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: -

Je, ni lini changamoto ya ukosefu wa Madaktari Bingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kitete itatatuliwa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Kitete hadi sasa ina jumla ya Madaktari Bingwa watano, ambapo Daktari Bingwa wa Afya ya akina mama na Uzazi mmoja, Madaktari Bingwa wa Watoto watatu na Daktari Bingwa wa Upasuaji ni mmoja.

Mheshimiwa Spika, katika kuongeza idadi ya Madaktari Bingwa, Wizara imepeleka kusoma jumla ya Madaktari - sita kutoka hospitali ya Rufaa ya Kitete ambao Madaktari - wawili wanasomea ubingwa wa magonjwa ya ndani, Daktari wa Magonjwa ya Kinywa, Sikio na Koo - mmoja, Ubingwa katika Mionzi ni mmoja, Ubingwa katika magonjwa ya dharura mmoja na Daktari Bingwa wa Afya ya akina Mama na Uzazi ni mmoja.

Mheshimiwa spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)