Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, ni lini changamoto ya ukosefu wa Madaktari Bingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kitete itatatuliwa?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, mwaka jana Bunge la Bajeti kama hili niliuliza swali kama hili hili na Mheshimiwa Naibu Waziri Dkt. Mollel mwenyewe aliniahidi mwaka jana kwamba ifikapo mwezi Novemba, mwaka jana wangekuwa wametuletea Madaktari Bingwa pale Kitete kwa sababu kuna upungufu wa Madaktari Bingwa wasiopungua 11.

Je, ahadi hiyo wale wananchi wa Tabora Mjini na especially kwa hiyo Hospitali yetu ya Kitete lini watapelekewa hao Madaktari Bingwa ambao niliahidiwa mwaka jana?

Swali la pili, hospitali ya Kitete ambayo ndiyo Hospitali yetu ya Rufaa ina upungufu mkubwa wa vifaa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa zikiwemo oxygen cylinders kwa wale wenye mahitaji maalum ya kupumua na vitu vinavyofanana na hilo.

Je, ni lini Serikali itatusaidia vifaa hivyo katika Hospitali yetu ya Rufaa ya Kitete? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mheshimiwa Mbunge aliuliza swali kama hili na Mheshimiwa Waziri wa Afya alielekeza kwamba wakati tunasomesha hawa, Madaktari wengine watafute sehemu zingine ili wapelekwe na ilishafanyika upembuzi yakinifu na wamepatikana Madaktari wa kusambazwa siyo tu Kitete ni maeneo mengi ya nchi ambayo kuna tatizo kama hili la Tabora.

Mheshimiwa Spika, sasa tupo kwenye stage ya kutafuta fedha kwa ajili ya uhamisho ili waweze kupelekwa kwenye maeneo yale, kwa kweli tumefikia karibia hatua za mwisho ili jambo hili liweze kutekelezwa ambalo ulitaka lifanyike.

Mheshimiwa Spika, swali lako la pili, kwanza ninakupongeza wewe na Wabunge wa Tabora kwa sababu mmepigana, lakini Rais wetu kwa mwaka huu kwa miaka yake hii miwili zimepelekwa Bilioni 13 kwenye hospitali yenu ya Mkoa. Maana yake unapozungumzia oxygen, kimejengwa kiwanda cha kuzalisha oxygen chenye thamani ya milioni 800 na sasa imeshawekwa miundombinu yote jengo limejengwa, kiwanda kimejengwa na imebaki tu filling pump ambayo mpaka tarehe 25 itakuwa imekamilika ili oxygen iweze kupatikana kwa ajili ya watu wetu wa Kitete.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, ni lini changamoto ya ukosefu wa Madaktari Bingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kitete itatatuliwa?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, mwaka jana mwezi Aprili ilikuwa, wakati tuko kwenye Bunge la Bajeti kama hivi, niliuliza the same question na Mheshimiwa Dkt. Godwin Oloyce Mollel bahati nzuri naye ndiyo bado Naibu Waziri wa Afya, walinijibu mpaka mwezi wa Kumi na Moja ule upungufu wa Madaktari Bingwa 11 ambao ulikuwepo mwaka jana hospitali ya Kitete na mpaka sasa hivi bado upo, kwamba wangeweza kuwa wameweza kutupunguzia mpaka mwezi wa Novemba, 2022 bado mpaka sasa hivi.

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ninamshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu mazuri na nimshukuru sana Mheshimiwa Mwakasaka kwa swali lake kuhusu ni lini Serikali itapeleka Madaktari Bingwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Kitete.

Mheshimiwa Spika, mwaka jana tulipata kibali cha ajira cha kuajiri Madaktari Bingwa lakini hatukuwapata sokoni, kwa hiyo mkakati tunautumia Serikali ni kama alivyoeleza Naibu Waziri ni wale ambao tayari ni Madaktari katika hospitali husika tunawapeleka kuwasomesha, na bahati mbaya hawajamaliza kusoma. Hatua ya haraka ambayo tumeifanya Mheshimiwa Mwakasaka, tumefanya tathmini ya Madaktari Bingwa tumegundua katika baadhi ya hospitali za Rufaa za Mikoa kuna Madaktari Bingwa wengi kuliko katika baadhi ya hospitali nyingine. Kwa hiyo, tunafanya re-distribution tunawatawanya upya, tumekwama tu kidogo kwenye fedha.

Mheshimiwa Spika, mwaka huu pia tumepata kibali cha ajira, tutaajiri Madaktari Bingwa na pia tutawasambaza katika Hospitali za Rufaa za Mikoa. Changamoto waliomaliza kidogo ni wagumu kuingia sokoni kwa hiyo mkakati tunaoutumia ni kuhamasisha Madaktari katika hospitali zetu za Rufaa za Mikoa wakasomee Udaktari Bingwa halafu wakirudi wabaki pale pale katika hospitali zao.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

SPIKA: Mheshimiwa Waziri ahsante sana kwa majibu yako. Naomba kuelewa wanasomeshwa na Serikali ama wanatiwa moyo ili wakajisomeshe wenyewe kwenye huo utaalam wa ziada.

WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ni swali zuri. Kipekee tunampongeza sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, kwa mara ya kwanza tumeanzisha utaratibu unaitwa Samia Suluhu Super Specialist Program tunasomesha Madaktari Bingwa zaidi ya 400 ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, tumeenda mbali hatuwasomeshi mmoja mmoja tunawasomesha katika utaratibu wa set, kama ni Daktari Bingwa kwa ajili ya upasuaji wa mifupa kwa hiyo anakwenda Daktari Bingwa Upasuaji wa Mifupa, anakwenda Nurse kwa ajili ya ICU - Intensive Care Unit, anakwenda Mtu wa Usingizi na anakwenda Mhudumu. Kwa hiyo, tunasomesha katika ngazi ya set na tunampongeza sana Rais Samia, tunayo bajeti ya kama bilioni nane na wiki ijayo tutakuja Bungeni kuomba tena bajeti Wabunge mtupitishie kwa ajili ya kusomesha Madaktari Bingwa nchini, ahsante sana.