Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 9 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 120 2023-04-18

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE K.n.y. MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kubadilisha Sheria ya Mirathi ya Kiserikali ya mwaka 1925 na Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria napenda kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Elias Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala la mirathi hushughulikiwa na sheria tofauti Tatu ambazo ni Sheria ya Kiislam, Sheria ya Kimila na kwa wale wasiotumia sheria hizo, Sheria ya Mirathi ya India ya mwaka 1925 (Indian Succession Act, 1925) ikiwa ni miongoni mwa sheria tulizorithi kupitia Sheria ya The Judicature and Application of Law (JALA) Sura ya 358.

Mheshimiwa Spika, aidha, sheria hizi katika kushughulikia suala la mirathi hutumika sambaba na Sheria ya Usimamizi wa Mirathi, Sura ya 352 ambayo ndiyo sheria mahsusi katika kushughulikia usimamizi wa mirathi yote nchi.

Mheshimiwa Spika, Wizara imeshaelekeza Tume ya Kurekebisha Sheria nchini kufanyia utafiti wa sheria zote zikiwemo Sheria za Mirathi ili kuziboresha na kuondoa vifungu ambavyo vinakiuka misingi ya haki na usawa. Kuhusu Sheria ya Ndoa, Serikali imeshaandaa mapendekezo ya marekebisho ya sheria hiyo na inatarajia kuyawasilisha katika Bunge hili linaloendelea. (Makofi)