Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE K.n.y. MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kubadilisha Sheria ya Mirathi ya Kiserikali ya mwaka 1925 na Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971?

Supplementary Question 1

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri kabisa ya Serikali, ninashukuru sana kwa uamuzi huu uliofikiwa sasa hivi, Mheshimiwa Waziri atakubaliana na mimi kwamba kuna mkanganyiko mkubwa hasa zaidi kwenye Sheria hizi mbili za Sheria ya Ndoa na Sheria ya Mtoto. Mtoto anatambulika chini ya miaka 18 lakini ndoa inaruhusiwa kufungwa akiwa na miaka 14. Kwa hiyo, ushauri wangu ni kwamba tunaiomba Serikali sasa ilete kwa haraka sasa sheria hii ili Wabunge tuweze kuipitia na kuifanyia marekebisho makubwa.

Mheshimiwa Spika, hoja yangu ya pili ni kwamba kumekuwa na usumbufu mkubwa sana kwa Wajane na Wagane hasa wanapofuatilia masuala ya mirathi na yenyewe hapa kwenye majibu ya Serikali wamasema watahakikisha wanaleta kwenye Bunge hili, tunataka tufahamu wakati mahususi kwa sababu sheria hii imepitwa na wakati ili iweze kujadiliwa na Wabunge na kupata matokeo mazuri. Ahsante. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika,
nakushukuru, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Cecil Mwambe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nakubliana nae kwamba Sheria hii ya Ndoa kuna baadhi ya vifungu ambavyo kwa kweli vimekuwa vikilalamikiwa hasa kile kifungu cha 13 na kifungu cha 17 ambazo zimetofautina katika umri wa mtoto wa kike kuolewa, lakini wakati mwingine Mahakama imekuwa ikitoa ruhusa hiyo pale wazazi wanapokuwa wameridhia, ndiyo maana Wizara tumeshakamilisha mchakato huu sasa tuwaleteeni katika Bunge hili tuweze kuamua na umri ambao utakuwa umependekezwa tutauona katika Muswada ambao tutauleta katika Bunge hili.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ameeleza kuhusu Wagane na Wajane ambao wamekuwa wakisumbuliwa katika masuala ya mirathi. Nimeeleza katika Sheria hizi ambazo zinasimamia mirathi ya kidini lakini pia wale ambao wanatumia Sheria hii ya Indian Succession nimeeleza kwamba taratibu hizi zipo lakini bado kuna malalamiko ndiyo maana Tume yetu ya Kurekebisha Sheria tumeiagiza pia ifanye utafiti watuletee. Katika Bunge hili tunategemea kuleta marekebisho ya Sheria zaidi ya 27.