Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 9 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 122 2023-04-18

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG'WASI D. KAMANI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaona haja ya kuondoa malipo ya Kodi kwa Wajasiriamali kabla ya kuanza rasmi kufanya biashara?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ng'wasi Damas Kamani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Muswada wa Sheria ya Fedha wa mwaka 2019, kifungu cha 43 imetoa unafuu wa kutolipa kodi kwa kipindi cha miezi sita kwa biashara mpya tangu mhusika anapopewa namba ya Utambulisho wa Mlipakodi. Lengo la hatua ni kumpa mjasiriamali nafasi ya kustawi kibiashara.

Mheshimiwa Spika, ahsante.