Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG'WASI D. KAMANI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaona haja ya kuondoa malipo ya Kodi kwa Wajasiriamali kabla ya kuanza rasmi kufanya biashara?

Supplementary Question 1

MHE. NG’WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Spika, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, la kwanza: Pamoja na Bunge lako hili Tukufu kupitisha Sheria hii ya Fedha mwaka 2019 inayotoa nafuu ya mjasiriamali kwa mtu anayeanza biashara kulipa kodi baada ya miezi sita, lakini bado wananchi wakienda kutafuta leseni kwenye Halmashauri zetu wanatakiwa kupeleka Tax Clearance kutoka TRA. Ili aipate hii Tax Clearance anatakiwa afanyiwe makadirio ya kodi na alipe kodi ya mwanzo. Sasa nini Kauli ya Serikali juu ya mkanganyiko huu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Sheria ya Uwekezaji Tanzania ikisomwa pamoja na Sheria mbalimbali za Kodi nchini, inatoa ruhusa kwa mamlaka mbalimbali za mapato kutoa msamaha wa kodi kwa wawekezaji wa nje mpaka mitano; na hii ni nzuri kwa ajili kukuza uwekezaji nchini. Sasa ni lini Serikali itaona haja ya kufanya mapitio ya Sheria hii ya Fedha ya mwaka 2019 ili kuongeza muda wa msamaha wa kodi kwa wazawa angalau kwa miezi 12 mpaka 18 ili: moja, kuendelea kutoa motisha kwa wawekezaji hawa wa ndani: na pili, kuwapa mazingira bora ya ushindani wawekezaji hawa wa ndani sambamba na wawekezaji hawa wa nje katika biashara? Ahsante. (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kamani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa idhini yako, naomba nielekeze Kamishna wa Mamlaka ya Mapato ya Tanzania kufanya kazi kwa mujibu wa Sheria. Sheria hii imepitishwa, hakuna Mjasiriamali yeyote mpya anayetakiwa kulipia chochote kabla ya biashara yake. Kwa hiyo, naomba nimwelekeze kufanya hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba nipokee maoni ya Mheshimiwa Mbunge tuyachukue kwenda kuyafanyia kazi.