Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 124 2023-04-19

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua Kituo cha Afya cha Laela na kuwa katika hadhi ya Hospitali ya Wilaya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya Laela kinamilikiwa na Kanisa Katoliki ambapo Mwaka 2004 kiliingia mkataba wa kutoa huduma na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ili kuhakikisha wananchi wa Kata ya Laela wanapata huduma za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, Serikali itatenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya kipya katika Kata ya Laela ambacho kitakuwa na uwezo wa kutoa huduma za afya pamoja na huduma za upasuaji za dharura.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga imeshajenga Hospitali ya Wilaya, Kituo cha Afya cha Laela kitatoa huduma kwa ngazi ya kituo cha afya, ahsante.