Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua Kituo cha Afya cha Laela na kuwa katika hadhi ya Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa fursa ya maswali madogo ya nyongeza. Kwanza, naishukuru Serikali kwa kukubali ombi hili na nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu aliahidi, wananchi wa Laela wanamshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza la nyongeza; Kata ya Ilemba ina wakazi wapatao 30,000 na ni miaka kumi sasa wanajenga kituo chao cha afya, hakijakamilika: Je, Serikali ina mpango gani wa kuunga juhudi za wananchi kukamilisha kituo hiki cha afya?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; Kata ya Msandamuungano kuna kituo cha afya ambacho kinajengo moja tu la OPD; Serikali ina mpango gani wa kuongeza majengo ili kiweze kutoa huduma zote zinazohitajika katika kituo cha afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata hii ya Ilemba ambayo ameitaja Mheshimiwa Mbunge ambayo wananchi wameanza ujenzi wa kituo cha afya; kwanza nitumie fursa hii kuwapongeza wananchi wa Kata hii kwa kuongeza nguvu zao katika ujenzi wa kituo hiki cha afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwahakikishie kwamba Serikali imeweka mpango mzuri wa kuunga nguvu za wananchi katika ukamilishaji wa majengo ya vituo vya afya na zahanati na tutaendelea kutenga bajeti na mara tukiwa na fedha hiyo, tutaona uwezekano pia wa kuchangia kukamilisha hicho kituo cha afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, kuhusiana na Jengo la OPD lililopo katika kituo hicho, ni kweli tuna vituo vingi vya afya vyenye majengo machache na vinahitaji kuongezewa majengo mengine, na mpango wa Serikali ni kuendelea kutafuta fedha na kupeleka kwenye majengo haya kikiwemo kituo hiki ili majengo yakamilike na kutoa huduma bora kwa wananchi, ahsante. (Makofi)

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua Kituo cha Afya cha Laela na kuwa katika hadhi ya Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kituo cha Njombe Mjini ni kituo kongwe katikati ya Mji, kimekuwa na ahadi za muda mrefu: Ni lini sasa kituo hiki kitapanuliwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Mwanyika, Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Kituo cha Afya cha Njombe Mjini ni kikongwe na ni chakavu, na pia kina miundombinu michache na Serikali imeshafanya tathmini ya uhitaji wa majengo ya ziada na kazi inayoendelea sasa ni kutafuta fedha ili fedha ikipatikana tukaongeze majengo yale na kukiwezesha kile kituo cha afya kufanya kazi inayotarajiwa, ahsante.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua Kituo cha Afya cha Laela na kuwa katika hadhi ya Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Wananchi wa Kata ya Narumu wameshatenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha afya cha Kata ya Narumu; je, ni lini Serikali itatuletea fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hiki cha Narumu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tuwapongeze wananchi wa Kata ya Narumu kwa ajili ya kutenga eneo kwa ujenzi wa kituo cha afya. Pia niwatie moyo kwamba waanze kwa nguvu zao kujenga kile kituo cha afya na baadaye Serikali ikipata fedha, basi tutakwenda kuwaunga mkono, ahsante. (Makofi)