Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 125 2023-04-19

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa maboma ya Ofisi Kata za Nkoma, Mwangudo, Mwamanimba na Imalaseko – Meatu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya, Mbunge wa Jimbo la Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua uwepo wa maboma manne ya Ofisi za Kata ya Nkoma, Mwangudo, Mwamanimba na Imalaseko katika Jimbo la Meatu ambayo yanahitaji kukamilishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Bajeti ya mwaka wa Fedha wa 2023/2024, Halmashauri ya Meatu imetenga fedha za mapato ya ndani kiasi cha shilingi milioni 60 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya Ofisi za Kata ya Imalaseko na Lingeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwenye vyanzo mbalimbali kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya ofisi za Kata nchini kote zikiwemo Kata za Nkoma, Mwangudo na Mwamanimba, ahsante.