Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa maboma ya Ofisi Kata za Nkoma, Mwangudo, Mwamanimba na Imalaseko – Meatu?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali kwa kutambua uwepo wa maboma nchini.

Je, Serikali haioni haja ya kutafuata programu nyingine ya kufanya maboresho katika Ofisi za Kata baada ya programu ya Ruzuku ya Uendelezaji Mitaji Serikali za Mitaa kukoma? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iliridhia watendaji walipwe shilingi 100,000; je, Serikali sasa haioni yale malipo yao yakakatwa at source, yakalipwa na Hazina katika mapato ya Halmashauri kwa sababu yanapitia kwenye mfumo wa Treasury Single Account ili kuondokana na usumbufu unaotokana na ucheleweshwaji wa Watendaji wa Kata kupata yale mafao? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya, Mbunge wa Jimbo la Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Ofisi za Maafisa Watendaji za Kata, na pia Ofisi za Watendaji wengine wote wa Serikali katika Halmashauri zetu na ndiyo maana imeendelea kutenga fedha kwa awamu, kuhakikisha kwamba tunakamilisha majengo hayo na fedha hizo ni kupitia mapato ya ndani, na pia kupitia fedha za Serikali Kuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nachukua fursa hii kuwakumbusha na kuwasisitiza Wakurugenzi wote wa Mamlaka za Serikali Mitaa kote nchini kuweka kipaumbele katika bajeti za mapato ya ndani kwa ajili ya Ujenzi wa Ofisi za Kata na pia Ofisi za Vijiji na Ofisi nyingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, kuhusiana na posho za Maafisa Watendaji wa Kata shilingi 100,000, Serikali ilishatoa maelekezo, na ni wajibu wa Wakurugenzi kuhakikisha fedha za posho za Watendaji wa Kata zinawafikia kwa wakati bila ucheleweshaji wowote. Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutafuatilia kuhakikisha kwamba fedha hizo zinawafikia kwa wakati, ahsante. (Makofi)

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa maboma ya Ofisi Kata za Nkoma, Mwangudo, Mwamanimba na Imalaseko – Meatu?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Swali langu ni kwamba; je, ni lini Serikali itapeleka fedha Wilayani Kilwa kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za Maafisa Watendaji Kata wa Kata za Somanga, Namayuni, Mitole na Njinjo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Ndulane, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshaelekeza kutumia fedha za mapato ya ndani kuanza Ujenzi wa Ofisi za Maafisa Watendaji wa Kata. Nitumie fursa hii kusisitiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilwa kutenga fedha kwa ajili ya Kata hizi za Somanga na Kata nyingine ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja, ili watendaji wetu wapate maeneo mazuri ya kufanyia kazi, ahsante sana. (Makofi)