Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 10 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 126 2023-04-19

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kudhibiti mafuriko katika Mto Mara kwa kuvuna maji kupitia Mabwawa na kujenga Skimu za Umwagiliaji?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jeremiah Mrimi Amsabi, Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais, tayari imezindua Mpango Kabambe wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (Environmental Master Plan for Strategic Intervention 2022-2032) ambao umeelekeza mikakati na shughuli endelevu zitakazoweza kufanyika katika maeneo hayo ni kama vile: kuimarisha usimamizi wa vyanzo vya maji na kuhakikisha uwepo wa mtiririko wa uhakika katika mito ikiwemo Mto Mara, Mto Kagera, Mto Ruaha Mto Wami na Ruvuma; kuhamasisha matumizi sanifu kwa watumiaji wote wa Mto Mara, Kagera, Ruaha, Momba na Mto Ruvuma; na kuimarisha viwango vya maji katika vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Mto Mara ni moja ya miongoni ya Mito mikubwa muhimu nchini Tanzania. Hivyo, Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais na Wizara nyingine za kisekta zitakaa na kuona namna bora ya kuvuna maji ili kudhibiti mafuriko, nakushukuru.