Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kudhibiti mafuriko katika Mto Mara kwa kuvuna maji kupitia Mabwawa na kujenga Skimu za Umwagiliaji?

Supplementary Question 1

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naishukuru Serikali kwa majibu mazuri. Hata hivyo, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza: Vijiji vya Borenga, Nyiboko, Buchanchali, Nyasulimunti na Gantamome ambavyo vipo kando kando ya Mto Mara kwa muda mrefu sasa vimeendelea kupata adha kubwa na hasara ya mafuriko katika mashamba, na tunaona mpango huu wa Serikali wa miaka kumi: Je, ni lini mpango huu utaanza ili kuondoa hadha hii inayoendelea katika maeneo hayo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kumekuwepo na mpango mzuri na maarufu kabisa wa Serikali uliojulikana kama Nile Basin Initiative ambao unahusisha maeneo haya ya Mto Mara kujengewa mabwawa makubwa, scheme za umwagiliaji na kudhibiti mafuriko haya: Je, mpango huu sasa wenyewe umefikia wapi? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jeremiah Amsabi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika Serikali hasa kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira tunayo nia ya kuhakikisha kwamba tunafanya huo mradi ambao Mheshimiwa ameupendekeza ama ameutaja. Kikubwa nimwambie Mheshimiwa awe na subira kwa sababu miradi hii kwanza lazima tufanye utafiti, tuone namna itakavyowezekana lakini lazima kuna Wizara tukae, kwa sababu kama tunavyoona hili jambo lina Wizara za kisekta lazima tukae Wizara ya Maji, tukae Wizara ya masuala ya Kilimo pia na sisi tukae pamoja, lakini kubwa zaidi atupe muda kidogo tutafute fedha kwa ajili ya kurekebisha ama kukamilisha mradi huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili nimwambie kwamba Wizara hii ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira tumekuwa tuna utaratibu wa kutembelea miradi takribani yote ambayo inasimamiwa na Ofisi yetu. Kila tunapokwenda tunatoa maelekezo kwamba kwanza miradi ikamilike kwa wakati, pili, miradi iwe ya kiwango, lakini tatu, miradi hii ihakikishe kwamba inanufaisha walengwa. Nimwambie tu kwamba miradi yote iliyo katika eneo lake ama jimbo lake tutaifuatilia na tutatoa maelekezo na itakamilika kwa wakati, nakushukuru.