Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 10 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 128 2023-04-19

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: -

Je, Serikali imejiandaaje kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji nchini?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema Kichiki Lugangira, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha kuna mazingira wezeshi Serikali imeendelea kutekeleza Mpango wa Kuboresha Mazingira ya kufanya Biashara Nchini (MKUMBI) lakini pia kuboresha sera na sheria mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia Bunge lako tukufu, Serikali ilitunga Sheria mpya ya Uwekezaji Tanzania ya mwaka 2022 ambayo pamoja na masuala mengine imeboresha na kulinda maslahi ya wawekezaji na uwekezaji, kuboresha huduma kwa wawekezaji katika kupata vibali na leseni mbalimbali kupitia mfumo unganishi wa kielektroniki katika kuhudumia wawekezaji, kuboresha utoaji wa vivutio vya kikodi kwa wawekezaji kwa kuongeza muda kutoka miaka mitatu hadi mitano na kutoa vivutio katika miradi ya upanuzi na ukarabati.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali pia inaendelea kuboresha miundombinu wezeshi kama barabara, reli, bandari, viwanja vya ndege na umeme, nakushukuru.