Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 10 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 130 2023-04-19

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: -

Je, ni lini Mafinga itanufaika na Mradi wa Umeme wa Peri-Urban?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya maeneo na Mitaa ya Mji wa Mafinga yatanufaika na Mradi wa Ujazilizi Awamu ya Pili C (Densification IIC) ambao upo katika hatua za ununuzi wa Wakandarasi. Aidha, Serikali imekamilisha uhakiki wa vitongoji visivyo na huduma ya umeme na kuandaa mradi kabambe wa kusambaza umeme katika vitongoji vyote uitwao Hamlet Electrification Project ambapo Mafinga Mjini nayo itanufaika na mradi huu. Mradi huu unatarajiwa kutekelezwa kuanzia Mwaka wa fedha wa 2023/2024 kulingana na upatikanaji wa fedha, nakushukuru.