Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, ni lini Mafinga itanufaika na Mradi wa Umeme wa Peri-Urban?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; je, Serikali wako tayari kukaa na mimi ili kuweza kufahamu hivyo vitongoji ambavyo vinaweza kunufaika na ujazilizi wa awamu ya pili unaoitwa IIC ni vitongoji gani na vingapi ili tuondoe mchanganyiko kwa sababu kuna wakati mwingine vitongoji vya Mafinga vinasomeka Mufindi na pale kuna Halmashauri ya Mji Mafinga na Halmashauri ya Mufindi. Kwa hiyo je, wako tayari kukaa na mimi ili tujue hivyo vitongoji?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; tunaipongeza Serikali kwamba maeneo ya vijijini bado wananchi wataingiza umeme kwa shilingi 27,000, lakini maeneo kama ya Mafinga yako maeneo pamoja na kuwa ni Mafinga Mji, lakini maisha, mazingira na kipato ni kama maisha ya kijijini.

Je, Serikali iko tayari maeneo kama hayo kama vile Ndolezi, Luganga na Ulole na wenyewe kuwapa bei nafuu katika kuingiza umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa David Chumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wetu wa Densification 2C utakuwa na una takribani vitongoji kama 2,562. Kama alivyoomba, na mimi niko tayari, baada ya hapa nitakaanaye ili nimuoneshe vitongoji ambavyo vitakuwa ni vya eneo lake kwa ajili ya kuhudumia wananchi katika Jimbo lake la Mafinga Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwenye swali la pili, kama ambavyo tumeeleza siku chache zilizopita, ni kweli Wizara ilituma timu yake kwenda katika majimbo yetu yote Tanzania ili kuhakiki yale maeneo ambayo yapo mijini, lakini yana uso wa vijiji ili kuweza kuwapangia bei ambayo ni stahiki na wanayoweza kulipa. Lakini kwa bahati mbaya taarifa tuliyoipata baada ya kui-verify humu Bungeni, tulibaini kuna Waheshimiwa Wabunge hawakushirikishwa. Kwa hiyo tumeiagiza ile timu irudi tena na kwenda kubaini upya hayo maeneo na ituletee taarifa. Hivyo taarifa hiyo itakapofika tutashirikishana hapa kwa ajili ya kuhakikisha kwamba, tunapanga bei ambayo wananchi wataimudu kwa ajili ya kuweza kuunganisha gharama za umeme.