Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 10 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 131 2023-04-19

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti matumizi holela ya Dawa za Binadamu nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko, Mbunge, Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kudhibiti matumizi holela ya dawa za binadamu nchini Serikali inatekeleza mambo yafuatayo: -

(i) Kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya dawa kwa wananchi kupitia vyombo vya habari ikiwemo vipindi vya elimu kwa umma kwa kutumia wataalamu wa dawa.

(ii) Kusimamia muongozo wa matibabu nchini unaobainisha matibabu kwa kila ugonjwa ikiwemo dawa zinazohitajika kutibu magonjwa hayo.

(iii) Kusimamia weledi wa watoa dawa katika maeneo yote yanayohusika na utoaji wa dawa kama vile maduka ya dawa na vituo vya kutolea huduma za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.