Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti matumizi holela ya Dawa za Binadamu nchini?

Supplementary Question 1

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi hii. Moja ya kisababishi kikubwa cha matumizi holela ya dawa za binadamu ni kukosekana kwa wafamasia kwenye vituo vya ngazi ya chini, kwa maana ya zahanati.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kusambaza wafamasia kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya nchini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; matumizi ya dawa holela yanaambatana au yanaenda sambamba na utengenezaji na usambazaji wa dawa holela. Hivi karibuni tumeshuhudia TMDA wamekamata watu mbalimbali wakiwa wanafanya shughuli hizo.

Je, Serikali sasa ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba, mambo hayo yanasitishwa na hayatokei tena kwa afya ya binadamu, Mtanzania?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge. Kwanza nimpongeze kwa sababu, swali lake ni muhimu sana na limekuja kwa wakati muhimu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza linasema ni kwa namna gani tunaweza tukahakikisha kwamba, vituo vyetu vya afya na zahanati kuna wafamasia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuwahakikishia kwamba, wafamasia, lakini tunaweza tukachukua wale waliosomea dawa, certificates na diploma. Tutashirikiana na wenzetu wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ili kuona kila wakati ni namna gani tutapunguza hilo gape kwa kuajiri watu wa namna hiyo ili kuweza kusimamia dawa vizuri kule chini.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali lake la pili ni kuhusu kwamba, kunakuwepo na utengenezaji holela wa dawa, kwa maana unamaanisha dawa ambazo ni fake: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza moja inaeleweka kabisa kwamba, tunayo taasisi yetu ya TMDA na inafanya kazi nzuri ya kuhakikisha hayo mambo hayatokei. Kikubwa tunaendelea, tunapoelimisha yote haya, elimu hiyo kwa jamii kwamba, watoe taarifa, tushirikiane kwa pamoja kuhakikisha tunadhibiti hawa wahalifu wanaofanya kazi hiyo, na kwamba wakipatikana wanapewa adhabu kubwa ambayo itawafanya wasirudie tena.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti matumizi holela ya Dawa za Binadamu nchini?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa zoezi la ukaguzi wa ubora wa dawa linafanyika katika vituo vya wauza dawa nchini, kitendo ambacho kinaleta hasara kubwa kwa wafanyabiashara hawa;

Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kuboresha mfumo wa udhibiti wa ubora wa dawa katika hatua za mwanzo kwenye viwanda ili wafanyabiashara wasipate hasara?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, moja ni kwamba, kwenye kudhibiti suala la dawa na wafanyabiashara ya dawa wenzetu wakati mwingine wanaangalia kutengeneza faida kuliko usalama wetu sisi watumiaji. Kwa hiyo suala la wao kuendelea kusimamiwa kwa nguvu na kuhakikisha kwamba wanafuata taratibu ni lazima tuwasimamie namna hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tumekuwa na mjadala wa kuhakikisha sasa badala ya kuwepo na wafamasia kwenye maduka ya dawa ambao wanaweka vyeti vyao, tubadilishe hiyo sheria iwe sasa mfamasia anaajiriwa kwenye duka husika na anakuweko pale kuhakikisha usalama unakuweko, na hasa kazi ya ukaguzi inakuwepo kwa mambo ambayo hayaendani na utaratibu yanazuiliwa mapema.

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti matumizi holela ya Dawa za Binadamu nchini?

Supplementary Question 3

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuna dawa ambazo zinanunuliwa bila cheti cha daktari, (over the counter medication) na kuna dawa zile ambazo ni lazima uwe na cheti cha daktari, ili uweze kununua, (prescription medication).

Je, Serikali inafanya jitihada gani na ina mikakati gani thabiti ya kuhakikisha kwamba, zile dawa ambazo zinahitaji cheti cha daktari hazinunuliwi over the counter? Yani, hazinunuliwi bila cheti cha daktari; na hasa kwa sababu, dawa za aina hii zinatumika na wale wenye uraibu wa dawa za kulevya?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Katimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, haya ni mambo ambayo tunakuwa tunaelimisha. Katika elimu hii tunayoitoa ni kuhakikisha kwamba watu wetu hawafanyi hivyo. Ukimsikia Mbunge mwenzetu akisema kuna baadhi ya maduka ya dawa ambayo tumekuwa tunawafungia na wamekuwa wakipewa adhabu mbalimbali, ni kwa sababu ya makosa kama hayo na kuna utaratibu wa kusimamia.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nataka kukuhakikishia tukienda sasahivi kuhakikisha kwamba maduka ambayo wafamasia waliopo wanaweka vyeti vyao badala ya kuweka cheti sasa wanaajiriwa wafamasia kwenye eneo husika, tutaondokana na matatizo kama hayo. Hii ni kwa sababu kwenye site atakuwepo mtaalamu wa dawa, atakuwepo na nesi ambaye ana utaalamu huo wa kuuza dawa na mambo mengine ambayo yatazuia hicho. Kwa sababu, hata kama ni duka la chini kabisa ni lazima anayeuza pale anajua dawa. Kwa hiyo, hayo matatizo yanadhibitika.