Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 9 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 132 2023-04-19

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kutoa bima za afya kwa wafungwa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Abdulkarim Halamga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa hakuna mpango mahususi wa bima ya afya kwa kundi la wafungwa. Katika kuhakikisha kuwa wafungwa wanapata haki yao ya msingi ya kupata huduma ya afya, Serikali imeweka utaratibu maalum wa kutoa huduma za matibabu kwa wafungwa katika magereza mbalimbali nchini kupitia vituo vya kutolea huduma za afya vya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inakamilisha Muswada wa Bima ya Afya kwa Wote, ambapo utakapokamilika utakuwa suluhisho la upatikanaji wa huduma za afya kwa makundi yote ya kijamii wakiwemo wafungwa. Naomba kuwasilisha.