Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutoa bima za afya kwa wafungwa?

Supplementary Question 1

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa kutoa huduma ya afya bure kwa wafungwa, lakini kwa kuwa Waziri amekiri kwamba, suluhisho la matatizo yote ya afya ni kupitishwa kwa muswada wa bima ya afya;

Je, changamoto wanazokutananazo kwa sasa wafungwa juu ya huduma za afya, Serikali haioni haja ya kukaa na kupitia utaratibu ambao imeuweka kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, lakini nianze kwa kusema kwanza ni wakati muafaka sisi Wabunge na sisi viongozi wote kujirudi na kutafakari kwa makini muswada wa bima ya afya kwa watu wote, moja hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa leo tu ukienda pale Mirembe wako wafungwa wa namna hiyo zaidi ya 270 na wanahudumiwa na wanapewa tiba bure na Serikali. Lakini pia, kweli kumekuwepo maeneo kama unavyosema Mheshimiwa Mbunge ambayo wakati mwingine akifika mfungwa anatakiwa kupewa huduma, anapewa zote bure, lakini kuna dawa inakosekana, saa nyingine ndugu anatafutwa kununua hiyo dawa iliyokosekana. Waziri wa Afya ameshatoa maelekezo kuhakikisha kwa kutumia watu wetu wa ustawi wa jamii mfungwa huyo anapitia kwenye utaratibu hata kwenye mapato ya ndani mfungwa huyo anatafutiwa dawa wakati tukishirikisna na Wizara ya Mambo ya Ndani kuona tunafanya nini, ili hilo tatizo lisiwepo.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutoa bima za afya kwa wafungwa?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Wakati tunasubiri Musawada wa Bima ya Afya kwa wote.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba, watu wenye ulemavu wanapata bima ya afya wasio na uwezo?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kumuomba Mbunge mimi nayeye ili tusisubiri muswada wa bima ya afya, tuusukume kwa pamoja tuhakikishe unatokea. Lakini pia, ukweli ni kwamba kila hospitali yetu anakuwepo mtu wa ustawi wa jamii. Kazi yake ni kuhakikisha watu wa namna hiyo wanashughulikiwa na wanapata huduma. Hao walemavu hakuna ambaye hana uwezo ambaye amekosa huduma.