Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 10 Water and Irrigation Wizara ya Maji 133 2023-04-19

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: -

Je, kwa nini Serikali isiingize gharama za mita za maji kwenye vitabu vyao vya fedha badala ya kuweka pale inapounganishwa maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu la Serikali ni kuhakikisha kunakuwa na dira za maji na kuwafungia wateja wanaoomba huduma za maji. Kwa kutambua changamoto za uunganishaji wa maji kwa wateja hususani kwenye suala la dira, Serikali imeandaa mwongozo wa ugharamiaji wa maunganisho ya maji vijijini ambao pia utajumuisha suala la dira za maji kuwa ni sehemu ya gharama za Serikali. Mwongozo huo utaanza kutumika mwezi Julai, 2023.